News
TCRA CCC Yatoa Elimu ya Usalama Mtandaoni kwa Walimu na Wanafunzi wa Sekondari Chenge Mkoani Simiyu
Katika kuendeleza juhudi za kutoa elimu kwa umma kuhusu matumizi salama ya huduma za mawasiliano, Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano (TCRA - CCC), kupitia Kamati ya Watumiaji Mkoa wa Simiyu, limeendesha mafunzo kwa wanafunzi na walimu wa Shule ya Sekondari Chenge iliyopo Kata ya Somanda, Bariadi Mjini.
Mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uelewa walimu na wanafunzi kama watumiaji wa simu janja kuhusu matumizi sahihi ya mtandao, huku yakisisitiza namna ya kujiepusha na changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika matumizi ya mtandao.
Miongoni mwa changamoto hizo ni pamoja na utapeli wa mtandaoni, unyanyasaji wa kimtandao, usambazaji wa jumbe za uongo na uchochezi, pamoja na ulinzi wa taarifa binafsi na usalama wa watoto mtandaoni.
Jumla ya washiriki 415 walihudhuria mafunzo hayo, wakiwemo wavulana 220, wasichana 186, na walimu 9.
Akizungumza katika tukio hilo, Mwenyekiti wa Kamati ya Watumiaji Mkoa wa Simiyu, Ndugu Faustine Juma Gomu, alisisitiza umuhimu wa kuwajengea wanafunzi uwezo wa matumizi sahihi ya mitandao ili iwasaidie katika maendeleo yao ya Kielimu.
βπππππ§π π€π π‘ππππππ ππππππ π ππ ππ ππππ π€π π’π πππππ ππ‘πππππππ, ππ π€πππππ’ππ§π πππ§πππ π€πππππππ βπ€π πππππ βππ‘πππ βπππππ€ππππππ πππ π€ππππππ π‘ππππ π πππππ π¦π ππ’π‘π’πππ ππ‘πππππ ππ€π πππππππππ π¦π πππππππ’ ππ πππππππ ππ€π π’ππ’πππ.β alisema Ndugu Gomu.


